Friday, June 26, 2009

MICHAEL JACKSON IS GONE

Mkali wa miondoko ya pop duniani ambae hakuna mwanamuziki aliewahi hata kujaribu kuvunja record yake kwenye mauzo na shows pia michael jackson aka wack jacko amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya UCLA baada ya moyo wake kusimama kufanya kazi.hakika atakumbukwa milele maana ni alikuwa mwanamuzi wa dunia.RIP wacko jacko.

MICHEAL JACKO COVERAGE


A mourner in Detroit.



Outside the Apollo Theater, the Rev. Al Sharpton, a friend of Mr. Jackson's, spoke to a crowd of people who were clutching the singer-dancer's pictures, playing his music and trying to imitate his signature moonwalk moves.

A fan reaction after get the horrybo new.












Members of the media and bystanders gathered outside the U.C.L.A. Medical Center in California, where Michael Jackson was rushed in a coma on Thursday. He was pronounced dead after arriving at the hospital in full cardiac arrest.




JAMANI HUU NDIO MWISHO WA COVERAGE YETU. DAH! JAMAA WE LOVED HIM BUT GOD LOVED HIM MO. RIP MICHEAL JACKO





Thursday, June 25, 2009

Mbunge: Wabunge wanafiki
Mbunge wa Viti Maalum, Lucy Owenya amesema, wabunge wanaowashambulia mawaziri halafu wanaunga mkono hoja ni wanafiki.
Owenya amesema bungeni mjini Dodoma kuwa, wabunge hao wameapa katika mhimili huo wa dola hivyo wanapaswa kutimiza kiapo chao.
Mbunge huyo amesema, wabunge hao wamekuwa wakisema sana, wanawalalamikia sana mawaziri halafu wanaunga mkono hoja.
Wakati Owenya anazungumzia aliouita kuwa ni unafiki wa wabunge alisema wawakilishi hao wa wananchi hawawatendei haki mawaziri na alitumia vifungu vya Biblia kuhalalisha hoja yake.
Mbunge wa Kibakwe, George Simbachawene, alipinga kauli ya Mbunge huyo kwa madai kuwa kusema kuwa wabunge ni wanafiki ni kuwadhalilisha.
Simbachawene amesema bungeni kuwa, kauli ya Owenya inaudhi na inadhalilisha watu wengine hivyo akaomba mwongozo wa Mwenyekiti wa kikao cha Bunge, Zubeir Ali Maulid.
“Na sio kuunga mkono kwamba ni upungufu na unafiki” alisema Simbachawene wakati akimpinga Mbunge huyo aliyekuwa akichangia wakati wa mjadala wa bajeti ya ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2009/2010.
“Kalindwa na Biblia, asitumie tena lugha hiyo inaudhi”alisema Mwenyekiti wa Bunge.
Mvutano huo ulitokea muda mfupi kabla Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto kutakiwa kufuta usemi kwamba Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Jeremiah Sumari alijibu honyo hovyo hoja kuhusu kampuni ya Meremeta.
Hivi karibuni, Mbunge wa Nzega, Lucas Selelii aliwashambulia mawaziri na kuwalaani kutokana na alichodai kuwa ni vitendo vyao vibaya.
Wabunge wamekuwa wakiwatuhumu mawaziri kuwa wanajipendelea na hawataki kuwahudumia wananchi wenye shida.
Wabunge hao wameahidi kumtajia Waziri Mkuu, Mizengo Pinda majina ya mawaziri wasiotekeleza wajibu wao na wanaokiuka misingi ya utawala bora.
Wabunge hao wamemsifu Waziri Mkuu kuwa ni muadilifu, na ana hofu ya Mungu. Mjadala wa bajeti hiyo iliyowasilishwa bungeni Jumatatu utahitimishwa leo.
Kwa mujibu wa Spika wa Bunge, Samuel Sitta, kabla wabunge hawajaanza kuchangia bajeti hiyo, zaidi ya wabunge 100 waliomba kuchangia lakini kwa sababu ya muda, takribani wabunge sitini tu ndiyo wangepata nafasi hiyo.